• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 8:55 PM
Kenya Shujaa yajikwaa 31-5 dhidi ya Afrika Kusini

Kenya Shujaa yajikwaa 31-5 dhidi ya Afrika Kusini

Na GEOFFREY ANENE

KENYA Shujaa imeanza duru ya tano ya Raga ya Dunia kwa kujikwaa mjini Los Angeles baada ya kuaibishwa 31-5 na miamba Afrika Kusini nchini Marekani, Jumamosi.

Vijana wa kocha Paul Feeney walipata mguso wa kujituliza roho kutoka kwa William Ambaka kabla tu ya kipindi cha kwanza kutamatika baada ya Afrika Kusini kupachika miguso miwili kupitia kwa Angelo Davids na JC Pretorius.

Werner Kok, Muller du Plessis na Branco Du Preez waliongeza miguso ya Afrika Kusini katika kipindi cha pili. Selvyn Davids, Cecil Afrika na Du Preez pia walichangia mkwaju mmoja kila mmoja.

Shujaa itakabiliana Ireland katika mechi yake ijayo saa saba usiku Machi 1, 2020 na kumaliza mechi za Kundi B dhidi ya Canada (5.35 a.m.).

Ireland ilichabanga Canada 17-12 katika mechi ya kwanza ya kundi hili.

Kenya ilivuta mkia katika duru ya nne mjini Sydney nchini Australia na inalenga kuepuka aibu hiyo mjini Los Angeles katika ligi hii ya duru 10 na mataifa 15 ambayo timu ya mwisho hutemwa.

You can share this post!

Christine Ongare anyakua tiketi ya kuchapana ndondi katika...

RIZIKI: Mwanadada anayesema ajira haihitaji mtu kujiuza...

adminleo