• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 6:27 PM
MAPISHI NA UOKAJI: Ivy Namulanda ni mpishi aliyetamani awe daktari wa maradhi ya ngozi

MAPISHI NA UOKAJI: Ivy Namulanda ni mpishi aliyetamani awe daktari wa maradhi ya ngozi

Na MAGDALENE WANJA

BI Ivy Namulanda alikuwa na ndoto ya kuwa daktari wa maradhi ya ngozi ili kuwasaidia watu wengi aliotangamana nao ambao walisumbuliwa na vipele, chunusi na matatizo mengineyo kama kuchubuka ngozi.

Hata hivyo, alipokamilisha elimu ya shule ya upili, ndoto yake ilionekana kuchukua mkondo tofauti.

Alitaka sana kuwa mpishi hodari ila ilimbidi – ilimlazimu – kujiunga na chuo kikuu ili asomee kozi ambayo ingewafurahisha wazazi wake.

Keki. Picha/ Magdalene Wanja

“Sikuwa na uhakika wa taaluma ambayo nilitaka kuisomea. Wakati mwingine, kuna baadhi ya watoto ambao huhitaji muda zaidi kuamua kile wanachokitaka maishani,” anasema Bi Namulanda.

Mwaka 2012 alijiunga na Chuo Kikuu cha Kilimo na Teknolojia cha Jomo Kenyatta (JKUAT) kufanya kozi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (IT) ambayo alifanya kwa muda wa miezi sita pekee lakini baadaye akagundua kuwa haikuwa ndoto yake kabisa.

Mnamo mwaka 2013, alijiunga na Chuo Kikuu cha Mount Kenya ambapo alifanya kozi ya Kuwahudumia Wateja – Hospitality Management – hasa katika maswala ya chakula na huduma za hoteli.

Keki. Picha/ Magdalene Wanja

“Ninapenda sana kupika na kugundua resipe mbalimbali. Nakumbuka hata nilipokuwa bado shuleni, ilinibidi kutumia njia za kale kama vile makaa ili kuoka mikate na keki,” anasema mpishi huyu.

Bi Namulanda sasa ana duka la kuoka mjini Nakuru ambapo anaandaa na kuuza aina mbalimbali za keki na mikate.

Duka lake kwa jina Pharaoh’s Cake House huwavutia wateja wa aina mbalimbali ama wa mitandaoni au wanunuzi wa wengine wanaofika hapo kufurahia aina mbalimbali za vyakula hivyo.

Keki. Picha/ Magdalene Wanja

You can share this post!

Mbunge wa Jomvu awaondolea wakazi hofu

Klabu za EPL kurejesha mabilioni kwa wapeperushaji wa mechi...

adminleo