• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 11:28 AM
SportPesa kufadhili FKF, KPL, Gor na Ingwe

SportPesa kufadhili FKF, KPL, Gor na Ingwe

Na BERNARDINE MUTANU

Hatimaye klabu za kandanda vya humu nchini zinaweza kusherehekea baada ya kampuni ya uchezaji kamari, Sportpesa kuingia katika mkataba nazo.

Pia watakaonufaika katika mkataba huo ni vyama vya humu nchini vya kandanda.

Kampuni hiyo ilitangaza kuingia katika mkataba huo wa Sh682 milioni siku chache baada ya Hazina ya Fedha kuchapisha mapendekezo ya kubadilisha sheria kuhusu ushuru unaotozwa kampuni za uchezaji kamari.

Katika pendekezo hilo, kampuni hizo huenda zikaruhusiwa ushuru wa asilimia 15 kutoka asilimia 35.

Kuambatana na mkataba huo, Ligi Kuu ya Kenya (KPL) itapata Sh295 milioni ilhali Shirikisho la Kandanda (FKF) litapata Sh69 milioni.

Vilabu vya Gor Mahia na AFC Leopards zipata Sh198 milioni na Sh156 kulingana na mfuatano huo.

“Tumetia sahihi mkataba wa miaka mitatu na FKF, KPL, Gor Mahia na AFC Leopards,” alisema Mkurugenzi Mkuu wa SportPesa Ronald Karauri Jumatatu wakati wa mkutano na wanahabari.

SportPesa mnamo Januari ilisitisha ufadhili wake wa vilabu vya kandanda baada ya serikali kuzitaka kampuni za uchezaji kamari kulipa ushuru wa asilimia 35.

You can share this post!

BI TAIFA APRILI 09, 2018

KRA yapungukiwa na Sh17 bilioni

adminleo