• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 5:55 AM
MAPISHI: Mahamri

MAPISHI: Mahamri

Na MARGARET MAINA

[email protected]

Muda wa maandalizi: Dakika 20

Muda wa mapishi: Dakika 40

Walaji: 5

Vinavyohitajika

Unga wa ngano vikombe 4

Sukari ¼ kikombe

Tui la nazi kikombe 1½

Mafuta ya kupikia

Hamira kijiko 1

Iliki kijiko cha chai 1

Unga wa maziwa vijiko 2

Maelekezo

Weka unga wa ngano kwenye bakuli uchanganye na maziwa ya unga au maziwa ya poda yaani powder milk.

Kwenye mchanganyiko huo, weka sukari, hamira, iliki, mafuta na tui na ukoroge mpaka sukari iyeyuke.

Changanya pamoja na unga mpaka vyote vichanganyike vizuri. Hakikisha unga hauwi mgumu na hauwi laini sana kama wa chapati.

Tengeza madonge ya kiasi, uyachovye kwenye unga kisha uyapange kwenye sahani na uyafunike.

Hakikisha madonge hayo unayapanga mbali mbali ili uyapatie nafasi ya kuumuka.

Yaache madonge kwa muda wa saa nzima mpaka yafure vizuri.

Bandika sufuria au kikaangio chenye mafuta ya kupikia motoni ili yaendelee kushika moto.

Sukuma mahamri na uyakate kwa shepu au maumbo upendayo. Pia usisukume donge sana mpaka likawa lembamba kama chapati.

Mahamri kabla kutumbukizwa kwa mafuta yakiwa na maumbo ya pembetatu. Picha/ Margaret Maina

Mafuta yakishika moto vizuri, weka mahamri yako na uyapike mpaka yawe na rangi ya kupendeza – kahawia – pande zote mbili.

Epua; yakipoa pakua na ufurahie.

You can share this post!

Wakazi wa Munyu na Komo kujengewa daraja jipya

Kindiki, Murkomen, Cherargei wakataa nafasi mpya walizopewa...

adminleo