• Nairobi
  • Last Updated March 19th, 2024 6:55 AM
Ratiba mpya ya EPL yatolewa

Ratiba mpya ya EPL yatolewa

Na CHRIS ADUNGO

RATIBA ya mechi 32 za kwanza kati ya 92 zilizosalia katika kampeni za Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) msimu huu imetolewa.

Kipute cha EPL kitarejelewa Juni 17, 2020 kwa mechi mbili zitakazokutanisha Aston Villa na Sheffield United kisha Manchester City na Arsenal. Mechi hizo ni zile zilizokuwa zimesalia kwa vikosi hivyo kucheza ili kufikia idadi ya michuano 29 ambayo wapinzani wote wengine 16 walikuwa wamepiga hadi kipute hicho kiliposimamishwa kwa muda kutokana na janga la corona mnamo Machi 13.

Mechi zote za raundi nzima ya 30 zimeratibiwa kusakatwa kati ya Ijumaa ya Juni 19 na Jumapili ya Juni 21, 2020.

Mechi za robo-fainali za Kombe la FA pia zitasakatwa wikendi ya Juni 27-28 amapo Norwich watawaalika Manchester United ugani Carrow Road nao Newcastle United wawe wenyeji wa Manchester City uwanjani St James’ Park mnamo Juni 27.

Sheffield United watawaalika Arsenal kabla ya Chelsea kuwaendea Leicester City ugani King Power mnamo Juni 28. Nusu-fainali za kipute hicho zitapigwa Julai 18-19 kabla ya fainali kushuhudiwa Jumamosi ya Agosti 1.

Mechi zote 92 za EPL zitapeperushwa moja kwa moja na SuperSport, Sky Sports, BT Sport, BBC Sport na Amazon Prime.

Gozi la Merseyside kati ya Everton na Liverpool ambalo huenda likawahakikishia vijana wa kocha Jurgen Klopp ufalme wa EPL kwa mara ya kwanza baada ya miaka 30 litasakatwa mnamo Juni 21.

Viwanja vitakavyotumiwa na Everton na Man-City kuwaalika Liverpool bado havijathibitishwa. Mechi kati ya Man-United na Sheffiled United ambayo maafisa ya polisi wanahofia itatawaliwa na vurugu kutoka kwa mashabiki nje ya uwanja itaandaliwa ugani Old Trafford.

RATIBA MPYA YA EPL:

Jumatano, Juni 17: Aston Villa na Sheffield United (8:00pm), Manchester City na Arsenal (10:15pm).

Ijumaa, Juni 19: Norwich na Southampton (8:00pm), Tottenham na Manchester United (10:15pm).

Jumamosi, Juni 20: Watford na Leicester City (2:30pm), Brighton na Arsenal (5:00pm), West Ham na Wolves (7:30pm), Bournemouth na Crystal Palace (9:45pm).

Jumapili, Juni 21: Newcastle na Sheffield United (4:00pm), Aston Villa na Chelsea (6:15pm), Everton na Liverpool (9:00pm).

Jumatatu, Juni 22: Manchester City na Burnley (10:00pm).

Jumanne, Juni 23: Leicester na Brighton (8:00pm), Tottenham na West Ham (10:15pm).

Jumatano, Juni 24: Manchester United na Sheffield United (8:00pm), Newcastle na Aston Villa (8:00pm), Norwich na Everton (8:00pm), Wolves na Bournemouth (8:00pm), Liverpool na Crystal Palace (10:15pm).

Alhamisi, Juni 25: Burnley na Watford (8:00pm), Southampton na Arsenal (8:00pm), Chelsea na Manchester (10:15pm).

Jumamosi, Juni 27: Aston Villa na Wolves (2:30pm).

Jumapili, Juni 28: Watford na Southampton (6:30pm).

Jumatatu, Juni 29: Crystal Palace na Burnley (10:00pm)

Jumanne, Juni 30: Brighton na Manchester United (10:15pm).

Jumatano, Julai 1: Bournemouth na Newcastle (8:00pm), Arsenal na Norwich (8:00pm), Everton na Leicester (8:00), West Ham na Chelsea (10:15pm).

Alhamisi, Julai 2: Sheffield United na Tottenham (8:00pm), Manchester City na Liverpool (10:15pm).

You can share this post!

Jadon Sancho atozwa faini kwa kunyolewa bila barakoa

Bayern yanusia ubingwa kwa mara ya 8 mfululizo

adminleo