• Nairobi
  • Last Updated April 23rd, 2024 1:08 PM
Jinsi unavyoweza kujitengenezea sabuni nyumbani

Jinsi unavyoweza kujitengenezea sabuni nyumbani

Na MARGARET MAINA

[email protected]

Muda wa kuandaaa: Dakika 30

Kiasi: Lita 25

Vinavyohitajika (Vitu hivi utavipata dukani kunakouzwa bidhaa za kutengenezea sabuni)

Maji lita 25

Kemikali ya Sulphonic

Manukato uyapendayo

Rangi (kijani/nyekundu au uipendayo)

Chumvi

Glycerin

Soda ash light

Formalin na alka.

Chombo chenye uwezo wa kuhifadhi zaidi ya lita 25

Maelekezo

Chukua sulphonic lita moja weka katika chombo chako cha kutengenezea (lita 25) kisha changanya na Slec.

Chukua soda ash nusu kilo kisha iloweke katika maji lita tano katika chombo kingine.

Ukishafanya hivyo, chukua mchanganyiko wako huo na umwagilie katika chombo chako chenye mchanganyiko wa sulphonic na Sles halafu mimina maji lita 15 na ukoroge kwa muda wa dakika 10.

Kisha weka rangi kiasi cha vijiko vitatu vya chai lakini angalia isizidi sana. Koroga tena vizuri.

Kisha chukua Glycerin vijiko viwili vya chai kisha weka katika mchanganyiko wako wa sabuni katika chombo chako.

Sasa ni wakati mwafaka wa kuweka kiasi unachotaka cha manukato yatakayofanya sabuni yako inukie vizuri.

Koroga chumvi pembeni; kiasi kidogo tu kama vijiko sita vya chai kisha mwagilia katika mchanganyiko wako na ongezea kiasi cha maji mpaka kufikia lita 25 .

TAHADHARI: Valia barakoa na glavu unapotengeneza sabuni hii na hakikisha unapata ushauri wa wataalamu wa kemikali na mamlaka za uhifadhi mazingira kama vile Nema nchini Kenya.

You can share this post!

Mzaha wa Dele Alli kuhusu corona wampokeza adhabu kali

Kiranja wa Wengi Machakos atimuliwa kwa kukosa nidhamu

adminleo