• Nairobi
  • Last Updated March 19th, 2024 11:34 AM
Ligi ya Super 8 yashika kasi

Ligi ya Super 8 yashika kasi

Na CECIL ODONGO

KLABU ya Shauri Moyo Blue Stars walitoka nyuma na kusajili ushindi wa kipekee wa mabao 2-1 dhidi ya mahasimu wao Zamalek FC katika mtanange wa ligi ya Super 8 uliovutia idadi kubwa ya mashabiki uwanjani Ziwani Jumapili.

Mshambulizi Papalai Morio aliifunga penalti safi dakika za majeruhi na kuwapa ushindi Shauri Moyo wanaoshikilia nafasi ya pili hii ikiwa ushindi wao watano mfululizo katika mechi saba walizosakata.

Timu hiyo sasa imezoa alama 16 wakiwa na upungufu wa alama nne ili kufikia viongozi Makadara Junior League SA.

Klabu hiyo kutoka mtaa wa Kamukunji walichukua uongozi wa mechi dakika ya tano kupitia mshambulizi Erick Kyalo mechi ikianza kabla ya wageni kusawazisha  kupitia ikabu ya Godfrey Gladson dakika tatu baadaye.

Kocha wa Blue Stars Ken Odera aliwapongeza wachezaji wake kwa kupigana hadi mwisho kupata ushindi huo.

“Nawapongeza vijana wangu kwa kudhihirisha soka ya juu na kupigana kufa kupona hadi mechi ikakamilika. Tunalenga kufanya vivyo hivyo katika mechi zijazo,” akasema Kocha Odera.

Kufuatia kichapo hicho Zamalek waliokuwa wakitafuta ushindi wao wa pili msimu huu wanashikilia nafasi ya 15 kwa alama tano na kocha wao Julius Katenge anaamini bado wana nafasi ya kuimarika.

“Tulipigana kiume na kusawazisha bao walilotufunga lakini matokeo yakawa vinginevyo. Tunalenga kujiimarisha kwenye mechi zijazo ili kuboresha matokeo yetu,” akasema baada ya mechi.

Viongozi wa ligi Makadara Junior League SA ndiyo walivuna pakubwa wikendi iliyopita baada ya kuandikisha ushindi wa kuridhisha wa mabao 5-0 dhidi ya Leads United uwanjani Camp Toyoyo.

Mshambulizi Tyrone Yara scored aling’aa kwa kufunga mabao matatu huku Zidane Ochieng’ na nahodha Billy Mutsami wakifunga bao moja kila moja kudumisha mwanya wa alama nne uongozini.

Katika matokeo mengine timu ya Makongeni Sports Association (MASA) Jumamosi ilipitia fedheha baada ya kucharazwa mabao 2-0 na Jericho All-Stars ugani Camp Toyoyo.

Vijana wa Chuo Kikuu cha TUK walipoteza 4-2 dhidi ya RYSA na kuzidi kusalia mkiani mwa jedwali.

Na kwenye uwanja wa Posta mjini Ngong NYSA waliwalambisha sakafu Melta Kabiria kwa mabao 3-2.

You can share this post!

Ni udhalimu kuongeza bei ya mafuta taa, Wakenya walia

Jombi ageuzwa gumzo mtaani kwa kuoa ajuza

adminleo