• Nairobi
  • Last Updated March 18th, 2024 8:55 PM
Wiper yaishtaki ODM kuhusu uongozi bungeni

Wiper yaishtaki ODM kuhusu uongozi bungeni

Na Collins Omullo

MVUTANO kuhusu wadhifa wa naibu kiongozi wa wachache katika Bunge la Kaunti ya Nairobi umechukua mkondo mpya, huku chama cha Wiper kikishtaki ODM kwa jopo la kutatua mizozo ya vyama vya kisiasa.? 

Wiper ilikimbilia kwa jopo hilo baada ya diwani wake, Bw Patrick Musili, kupokonywa wadhifa wa naibu kiongozi wa wachache.

Nafasi hiyo ilipokezwa diwani maalum wa ODM, Melab Atema.Bw Musili ambaye ni diwani wa Wadi ya Hospital, alilitaka jopo hilo kusitisha utekelezwaji wa mabadiliko hayo ya uongozi yaliyofanywa na chama cha ODM mnamo Agosti 18, mwaka huu, hadi kesi hiyo itakaposikilizwa na kuamuliwa.

Jopo hilo linaloongozwa na Bi Desma Mungo, lilikubaliana na ombi lake na kusitisha kutekelezwa kwa mabadiliko hayo hadi kesi hiyo itakapoamuliwa.

Agizo la jopo hilo la kusitisha mabadiliko hayo lilitolewa Agosti 25, mwaka huu. Kesi hiyo itatajwa Septemba 8, mwaka huu, kuthibitisha ikiwa maagizo yaliyotolewa na jopo hilo yalitekelezwa.

You can share this post!

Wajane wazee walia kubakwa na vijana usiku

Ruto aongoza wimbo akirejea kanisani kwa kishindo