• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:42 PM
WATOTO: Ujasiri wa kuwa mwanamitindo kuanzia umri mdogo

WATOTO: Ujasiri wa kuwa mwanamitindo kuanzia umri mdogo

Na PHYLLIS MUSASIA

Clara Mereso ni mwanafunzi wa Darasa la Kwanza katika shule ya Melvin Jones Lions Academy mjini Nakuru.

Msichana huyo mwenye umri wa miaka sita ana uraibu katika maswala ya unamitindo ambao alianza akiwa na miaka mitatu.

Hadi sasa, ameweza kushinda mataji matatu ikiwemo, Little Miss Peace Nakuru, taji ambalo alishinda mnamo mwaka wa 2017, Tiny Miss Kenya Nakuru, mnamo 2018 na Tiny Miss World Kenya mnamo 2019.

Ujasiri alionao umemwezesha kupata fursa ya kushiriki katika matangazo ya bidhaa za kampuni ya Dura Coat pamoja na mashindano ya Rosy.

Mereso amewai pia kushiriki katika tamasha za wasanii ambazo zilihusisha watoto kama vile Churchil Kids Festival na makaribisho ya msanii Avril nyumbani kwao Nakuru.

Taifa Leo Dijitali ilipokutana naye nyumbani kwao katika kaunti ndogo ya Nakuru Mashariki, Mereso alisema kuwa hatolegeza Kamba katika ndoto yake ya kuwa mtunza amani atakapokuwa mkubwa.

Kulingana naye, mamake amekuwa wa msaada sana katika juhudi zake licha ya umri wake. Katika kushinda taji zote, mamake amemwelekeza na kumshauri vilivyo.

“Ninaamini kuwa nilizakuwa kuwa mshindi na nitafanya bidii kuhakikisha kuwa ninashinda katika kila jambo nitakalo shiriki,” akasema.

Aliongeza kuwa, “mama amenifunza kuwa mvumilivu, kumtegemea Mungu na kuamini kuwa kila jambo linawezekana.”

Mereso anaamini kuwa yeye ni msichana mrembo na mwenye akili zaidi ulimwenguni.

Clare Mereso mwenye umri wa miaka 6 ni mwanafunzi wa gredi ya kwanza katika shule ya Melvin Jones Lions Academy mjini Nakuru. Yeye ni mwanamitindo na ameshinda tuzo tatu tangu 2017. Picha/ Phyllis Musasia.

Aidha, anatazamia kushinda taji zaidi siku zijazo.

“Nilipokuwa na umri mdogo kuliko sasa, watu wengi walinieleza kuwa mimi ni mrembo na hadi sasa bado wao husema hivyo. Wakati huo, sikuelewa walimaanisha nini lakini leo hii, ninazidi kujifunza jinsi ya kufanya makuu ili mafanikio yangu iandamane zaidi na urembo wangu,” akasema.

Kabla kuzuka kwa janga la corona, Mereso alishiriki katika mafunzo ya modeli kila Jumamosi katika shule ya Little Big Talents ambayo huendesha shughuli zake katika hoteli ya Kunste mjini Nakuru.

“Mwalimu wangu anaitwa Bi Joan Musumba na amenifunza mambo mengi sana. Ana fadhili na ni mkufunzi bora zaidi kati maswala ya modeli ya watoto,” akasema Mereso.

Wakati huu wa janga, Mereso hutumia wakati wake mwingi kusoma akiwa nyumbani kupitia mtandao wa zoom.

Anajifunza pia kuhusu nyimbo katika mtandao kwa kutumia simu ya mkononi ya mamake.

“Kila wakati niapokuwa nimemaliza masomo ya siku, mimi hujihusisha katika kusikiza mziki na kujifunza kuimba kwa sauti nzuri. Ningependa pia kuwa msanii wa nyimbo za kuhubiri amani,” akasema.

Tayari Mereso anasaidiwa na mamake kutunga wimbo ambao unahusu usalama wa wototo wakati huu wa janga la Covid-19.

Kulingana naye, wakati huu ambapo hafla na sherehe zimesitishwa ili kuzuia maambukizi ya Covid-19, kutangamana na watoto wengine imekuwa vigumu na ndio sababu anatunga wimbo ili kuwafikia wengi mahali ambapo walipo.

Anasema kupitia wimbo huo atatumia mitandao za kijamii kama vile Facebook na Youtube ili kuwasilisha ujumbe wake.

“Wakati huu ambapo siendi katika mafunzo, mama yangu ndio mwelekezi na anafanya kazi nzuri. Ananipa mifano ya watu ambao walianza kama mimi na sasa wamefaulu. Ananishauri pia nikaze mwendo,” akasema Mereso.

Licha ya kwamba, Mereso anauraibu katika maswala mbalimbali, masomo yatasalia kuwa kipaumbele siku zote.

You can share this post!

Wandani wa Ruto sasa wamuonya Murathe

Wakulima waililia kaunti iwachimbie mabwawa