• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:00 PM
ULIMBWENDE: Jinsi ya kuondoa weusi makwapani

ULIMBWENDE: Jinsi ya kuondoa weusi makwapani

Na MARGARET MAINA

WEUSI makwapani ni mabadiliko ya ngozi yanayotokea na hufanya watu wengi wasiwe na starehe wakivaa nguo za wazi mbele za wenzao.

Hali hii husababishwa na kunyoa mara kwa mara, seli zilizokufa, mtu anapotumia ‘deodorant’ yenye pombe inayobadili rangi, matumizi ya creams za kunyolea (kupakwa makwapani), kikwapa (yaani jasho la kwapani), kuvaa nzuo nyingi au nzito, na mwili kukosa hewa vizuri.

Vipo vitu vya asili unavyoweza kutumia kumaliza kabisa hali hii 

Unaweza ukatoa weusi huo kwa kutumia vitu ambavyo havina kemikali (au visivyo na kemikali zenye athari hasi) kama vile;

  • Limau

Chukua limau au ndimu na ukate vipande vya mduara. Kwa vipande hivi paka sukari au asali juu yavyo na kisha chukua hivyo vipande ujipake makwapani mara mbili kwa siku.

Wakati unapaka unashauriwa uache kwa dakika 10 kabla ya kuoga.

Baadaye osha kwa maji ya fufutende (luke warm).

Limau inatumika kama ‘bleach’ kutoa hiyo rangi na kutoa seli zilizokufa kwenye hiyo ngozi ya kwapani.

  • Hamira (Baking soda)

Inasaidia kutoa seli zilizokufa kwa urahisi.

Changanya baking soda na maji iwe nzito na kisha paka kwapani. Acha kwa dakika 10 halafu osha na jikaushe. Fanya hivyo mara 2-3 kwa wiki.

Unashauriwa kuendelea na shughuli hiyo mpaka utakapoona umeridhika na mabadiliko.

  • Maganda ya machungwa

Chukua maganda ya machungwa na uyakaushe juani. Yakishakauka yaponde, changanya na maji ya waridi (rose water) na ukoroge.

Kwenye mchanganyiko ongeza maziwa na uanze kupaka makwapani kwa dakika 10-20. Baada ya kufanya hivyo, unaweza kuosha makwapa.

  • Viazi

Menya viazi kisha vikate vipande, jipake makwapani yale maji yake yakiingia kwenye ngozi yanatoa rangi nyeusi au unaweza kuponda kikiwa kibichi na kujipaka kwa dakika 10-20 kisha nawa. Unaweza kufanya hivyo mara mbili kwa siku mpaka weusi utakapoisha.

  • Tango (cucumber)

Kata vipande vya tango na ujipake kwapani. Yale maji yake ndiyo dawa. Unaweza pia kuvisaga vipande hivyo viwe nyororo ndipo upake; acha kwa dakika kati ya kumi na ishirini.

  • Sukari

Chukua sukari uchanganye na mafuta ya mizeituni; paka na baada ya muda osha.

  • Mafuta ya nazi

Mafuta haya yana vitamini E na yanasaidia kung’arisha ngozi.

Jipake makwapani na baada ya dakika 10-20 hivi, osha makwapa yako kwa maji moto.

Shughuli hii inaweza kuchukua muda mchache ukaona mabadiliko makubwa au ikachukua muda mrefu mpaka uone mabadiliko; inategemea ngozi ya mtu.

You can share this post!

Ziara ya ghafla ya Rais Kenyatta kaunti ya Lamu

Tumbojoto bungeni kuhusu ombi la Ouda kutaka Ruto asiwanie...

adminleo