Michezo

Chelsea yasajili kipa mpya raia wa Denmark


KLABU ya Chelsea imesajili kipa Filip Jorgensen kutoka klabu ya Villarreal kwa mkataba wa miaka saba ambao uligharimu Sh2.7 bilioni.

Raia huyo wa Denmark alivutia vigogo hao wa Ligi Kuu ya Uingereza baada ya kung’ara kama mlinda lango chaguo la kwanza wa klabu ya Villarreal msimu uliopita.

“Nimefurahia kujiunga na Chelsea, mojawapo wa klabu kubwa zaidi duniani. Ndoto yangu ya muda mrefu imetimika,” alisema mlinda lango huyo mwenye umria wa miaka 22.

Hata hivyo, kipa huyo atahitajika kupigania namba na Robert Sanchez aliyekuwa kipa chaguo la kwanza wa klabu hiyo ya Ligi Kuu ya Uingereza (EPL).

Kipa huyo aliyezaliwa Sweden aliwakilisha Denmark katika mashindano mbali mbali ya kimataifa ya umri tofauti hadi ya wachezaji wasiozidi umri wa miaka 21.

Alijiunga na Villarreal akiwa na umri wa miaka 25 na kupanda hadi alipopata nafasi ya kuchezea timu kuu ya taifa mnamo Januari 2023.

Tayari mlinda lango huyo ametua Califonia nchini Amerika kujiunga na wenzake katika kambi ya mazoezi kwa ajili ya msimu mpya wa 2024/2025.

Chelsea wamebakisha mechi tatu za maandalizi dhidi ya Club America, Manchester City, Real Madrid kabla ya kurejea London juma lijalo.

Mabingwa hao mara sita wa EPL mara sita (1955, 2005, 2006, 2010, 2015 na 2017) wamepangiwa kuanza msimu dhidi ya Manchester City mnamo Agosti 18, ugani Stamford Bridge.