Aliyefutwa aangukia mikononi mwa mumama mali safi baada ya mkewe kumfurusha
MWANADADA wa Changamwe, Mombasa alijuta kumtimua mumewe kutoka nyumbani kwake alipopoteza kazi.
Jamaa alichukuliwa na mama mmoja tajiri ambaye hakuwa na mume na akamtunza kama mfalme.
Mama huyo alimpata jamaa nje muda mfupi baada ya kutimuliwa na mkewe aliyekuwa akilipa kodi ya nyumba na kukidhi mahitaji yote kwa miezi sita huku jombi akisaka kazi bila mafanikio.
Mama huyo alimhurumia jamaa na kumkaribisha kwake akampa chumba akalala usiku huo.
Siku iliyofuata, alimwambia alikuwa tayari kumtunza bila kero kama aliyopata kwa mkewe na jamaa akakubali na wakaanza kuishi pamoja.
Mkewe amekuwa akijuta kwa kuwa japo jamaa hajapata kazi, anatunzwa vizuri na ametulia.