Dondoo

Binti aonya mamake akome kuchekacheka na mume wake

Na MWANDISHI WETU August 20th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

KATIKA tukio lisilo la kawaida,msupa mmoja wa hapa alimpigia mamake simu na kumuonya vikali akome kucheka cheka na mumewe kila mara.

Mwanadada huyo alishuku kwamba wawili hao walikuwa kwenye uhusiano wa kisiri baada ya jamaa kutoa usemi kwamba mama-mkwe alikuwa amedumisha urembo wake.

Matamshi hayo yalimshtua mwanadada huyo aliyehisi kwamba mumewe alikuwa na lengo la kunyemelea mama mkwe.

Demu akikasirika zaidi aliporejea nyumbani juzi na kupata mamake mzazi akiongea na mumewe kwa ‘video call’ huku wakicheka cheka.

Alimfokea mumewe akimlaumu kwa kuvuka mipaka na kukosa utu.

“Nilidhani wewe ni mtu unayejua mipaka kumbe huna heshima hata kidogo.Unawezaje kumrushia mama-mkwe mistari? Sikujua mamangu mzazi pia anaweza kunisaliti kiwango hiki,” alilia kabla ya kuchukua simu na kumpigia mamake kumtaka akome kumharibia ndoa.