Dondoo

Demu azua kizaazaa kugundua mumewe hakumweka kwenye orodha ya warithi wa mali yake

Na BENSON MATHEKA February 5th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

WANGIGE, KIAMBU

KIZAAZAA kilizuka katika boma moja eneo hili mwanadada alipomfokea mumewe baada ya kutambua hakuwa amemjumuisha katika orodha ya watakaorithi mali yake.

Inasemekana jamaa na mwanadada walikuwa na migogoro ya kila mara katika ndoa yao hali iliyofanya jamaa kutokuwa na imani na mkewe.

Ilibainika kwamba jombi alikuwa ametaja jamaa zake pekee kuwa warithi wa mali yake kwa kuwa yeye na mkewe hawakuwa wamejaliwa watoto.

Japo haikujulikana alivyopata orodha hiyo demu alilipuka kwa hasira alipogundua hakuorodheshwa kurithi mali ya jamaa.

“Sasa nimejua hunitambui kama mkeo. Nimeamini huna mapenzi ya dhati kwangu lakini upende usipende lazima nitaridhi mali yako. Mimi ni mkeo halali,” mke wa jamaa alisema naye akasisitiza hangemlazimisha amwachie mali ambayo hajukumiki kutunza.

Alidai demu anapenda kulaza damu tu na kula kama mchwa.