Familia yakosa usingizi Kitui ikidai kusikia milio, vyombo kusonga vyenyewe
IKUTHA, Kitui
HOFU ilitanda katika kijiji kimoja hapa baada ya familia kudai kuvamiwa na nguvu zisizoeleweka usiku wa manane.
Watu wa familia walipiga nduru wakidai walisikia milio ya ajabu, vitu kusonga vyenyewe na sauti zisizoeleweka hali iliyowafanya kuingiwa na wasiwasi mkubwa.
Wanakijiji walikusanyika kwa wingi na kumtuhumu mzee mmoja kuwa chanzo cha matukio hayo, wakidai ana historia ya kujihusisha na masuala ya giza.
Hata hivyo, viongozi wa eneo hilo waliingilia kati haraka na kuwataka wakazi kuacha imani potovu na kuchukua tahadhari kabla ya kumhukumu mtu bila ushahidi wa kutosha.