Jombi asalimisha mkewe na watoto kwa jirani akisema wanafanana zaidi kumliko
MTWAPA, KILIFI
POLO mmoja aliwaacha wengi vinywa wazi baada ya kuamua kumkabidhi jirani yake mkewe pamoja na watoto wake wawili akidai wanafanana naye kuliko yeye mwenyewe.
Walioshuhudia tukio hilo walisema jamaa huyo kwa muda mrefu alikuwa akidhihakiwa na wakazi mtaani wakidai watoto hao hawakufanana naye hata kidogo bali walikuwa sarafu kwa ya pili na jirani yake ambaye nyumba zao za kukodisha zinapakana.
Inasemekana jamaa huyo alijaribu kuvumilia kejeli kwa miaka mingi lakini siku hiyo alirejea nyumbani kutoka kazini akiwa mwenye mawazo mengi.
Mkewe alipomuuliza kilichokuwa kikimsumbua, alimwambia aandae watoto ili wawapeleke kwao.
Mkewe alidhani wanaelekea kijijini na akawaandaa watoto kwa haraka. Walipotoka nje, jamaa aliwaongoza hadi kwa nyumba ya jirani huyo.