Kalameni akesha kwa mpango wa kando akisingizia mafuriko
KILELESHWA, NAIROBI
WATU walipokuwa wakilalamikia mvua kubwa iliyozua mafuriko jijini polo mmoja mtaani hapa, aliitumia kama kisingizio ili akeshe kwa mpango wa kando.
Jamaa huyo aliondoka nyumbani jioni akidai anaenda kumtembelea rafiki aliyekuwa mgonjwa.
Hata hivyo, usiku ulipoingia mvua kubwa ilianza kunyesha, naye akapiga simu nyumbani akisema hangeweza kurejea kwa sababu barabara zilikuwa zimejaa maji na aliamua kulala kwa rafiki yake.
Mkewe hakutilia shaka sana kwa kuwa mvua ilikuwa ikinyesha kweli. Kumbe jamaa alikuwa amekesha kwa mpango wa kando mtaani Donholm.
Asubuhi ilipofika, siri ilifichuka demu huyo alipopakia chapisho kwenye mtandao wa kijamii akijigamba kuwa mvua ilikuwa baraka kwake kwa sababu ilimsaidia kukesha na mume wa mtu.
Mke wa jamaa anayefuatilia demu huyo katika mitandao ya kijamii alikuwa akishuku uhusiano wa polo na demu huyo aligundua mvua ilikuwa kisingizio cha kutorudi nyumbani.
Alimtumia ujumbe akimweleza kuwa mpango wake wa kando alimsaliti na kumtaka aendelee kuishi huko hadi msimu wa mvua uishe.
Jamaa alijaribu kujitetea kwa kusema mvua ndiyo iliyomzuia lakini hii maelezo yake hayakuwa na mashiko.