Dondoo

Kalameni akiri alijifanya mgonjwa ili amkatie nesi hospitalini

Na DENNIS SINYO September 24th, 2024 1 min read

KALAMENI mkazi wa hapa alishangaza watu alipofichua kuwa alijifanya mgonjwa ili akutane na nesi mmoja amrushie mistari.

Jamaa huyo anadai lengo lake lilikuwa kukutana na nesi huyo ili apate nafasi ya kumweleza anampenda.

Kauli ya jamaa ilichangamsha baadhi ya waliomsikiliza wakampongeza kwa ubunifu wake huku wengine wakimwambia alikosea kwa kujifanya mgonjwa.

“Mwanamume kamili hawezi kujifanya dhaifu ili kunasa demu, anajiwasilisha alivyo na kusuka mistari ya nguvu,” jumbi mmoja alimweleza.