Dondoo
Lofa aliyeiba chupa ya pombe anunuliwa kreti amalize

Mwanamume akibugia pombe. Picha|Maktaba
KOCHOLIA, TESO
MWANAMUME aliyekamatwa baada ya kufumaniwa akiiba chupa ya pombe alikuwa na wakati mgumu baada ya wateja kumnunulia kreti nzima ya pombe.
Inasemekana walinzi wa baa walimkamata akiiba pombe ya mteja aliyekuwa ameenda msalani kujisaidia.Jamaa ambaye ni lofa wa mtaa alianza kulia akiomba msamaha.
Alidai licha ya kuwa mraibu,hakuwa ameonja dozi wiki nzima. Kilio chake kilivutia wateja kwenye baa hiyo wakaamua kuchanga pesa na kumnunulia kreti nzima ya pombe.