Dondoo

Mafuriko yafanya demu amfokee mumewe kwa kutojenga ushago

Na RICHARD MUNGUTI March 23rd, 2026 Kusoma ni dakika: 1

TENA, NAIROBI

MVUA kubwa inayoendelea kunyesha jijini Nairobi wiki iliyopita ilisababisha mzozo mkali kati ya mke na mume baada ya mwanamke huyo kumtaka mumewe amjengee nyumba ya mawe mashambani.

Mama huyo wa watoto wanne alimlaumu mumewe kwa kuchelewa kujenga nyumba ya kudumu katika kijiji chao, akisema anaogopa mafuriko yanayozidi kuathiri baadhi ya maeneo ya jiji.

“Sitaki kufa mimi na watoto wangu. Turudi mashambani,” alikemea mumewe.