Maisha magumu yawasukuma dada wawili kushinikiza mama yao arudi kwa mume aliyemtaliki
Inasemekana mama huyo alitofautiana vikali na mumewe miaka miwili iliyopita kisha akaamua kubeba virago vyake na kuondoka kuanza maisha kivyake akiwa na binti zake.
Hata hivyo, maisha yalianza kuwa magumu kwake na wasichana hao waliomlaumu mama yao.
“Baba yetu alikuwa akitupa kila kitu tutakacho. Tuliishi maisha ya starehe na hatukukosa lolote. Sasa umetuleta hapa mahali kukavu na tunahangaika tu. Hata wale waliofanya ukosane na baba yetu wameshindwa kukutimizia mahitaji yako! Heri urudiane na baba, tuendelee na maisha yetu kama awali,” wasichana hao walimshauri mama yao. Haikubainika wazi iwapo mama huyo alirudiana na mumewe au la.