Dondoo

Mama arudi kwa ‘ex’ na kikosi cha watoto aliozaa nje ya ndoa

Na BENSON MATHEKA March 3rd, 2026 Kusoma ni dakika: 1

MAMA mmoja amerudi kwa mumewe wa zamani baada ya kutengana kwa miaka 15, akiwa na watoto wanne aliowazaa na wanaume tofauti katika kipindi hicho.

Inasemekana waliachana kutokana na migogoro ya kifamilia na changamoto za kiuchumi.

Baada ya kutangatanga na kujaribu mahusiano mengine bila mafanikio isipokuwa kuzalishwa na wanaume tofauti, mama huyo aliamua kurejea kwa mumewe wa kwanza akidai ametambua makosa yake na kutaka waanze upya.

Mumewe anaripotiwa kukubali kumpokea, lakini kwa masharti kwamba kila mtoto awajibikiwe na baba yake mzazi.

Sasa macho yote yako kwa wanandoa hao kuona kama wataweza kuvuka yaliyopita na kujenga upya ndoa yao.