Dondoo

Wazee wasusia harusi ya demu ‘aliyeokotwa’ mtandao wa kijamii

Na TOBBIE WEKESA October 7th, 2024 Kusoma ni dakika: 1

HOLA, TANARIVER

KALAMENI wa hapa hakuamini baada ya wazee na jamaa wa familia kukataa kuhudhuria harusi yake kwa madai kwamba alimtoa kidosho mtandaoni.

Wazee walidai kwamba polo na kidosho walikutana kwenye mtandao jambo ambalo halikuwafurahisha kabisa.

“Huyo msichana tumepata habari mlikutana mtandaoni. Picha zake tumeziona. Hazipendezi kabisa,” wazee walimueleza polo.

Polo alijaribu kujitetea lakini hakutoboa. Wazee waliapa kutohudhuria harusi.

“Huyu aliamua kujianika ili kuwavutia wanaume. Huyu si mwanamke wa kutuletea kijijini,” wazee walisema.

Wazee walidai kwamba polo hataweza kumdhibiti kidosho wakioana.