Habari za Kaunti

Gavana amlilia Ruto kumboreshea barabara

Na SAMMY KIMATU September 2nd, 2024 1 min read

WAKAZI wa Machakos wameiomba serikali ya kaunti hiyo kupitia kwa Gavana Wavinya Ndeti kukarabati barabara iliyoharibiwa na mvua na sasa ina mashimo mengi.

Wakazi wa kijiji cha Ngelani, Kivutini, Kithima, Kisekini, Kasovya na kijiji cha Thinu wanalalamikia hali mbaya ya barabara ya Ngelani-Kivutini.

Barabara hiyo ni muhimu kwani huunganisha vijiji sita na barabara kuu ya Kangundo-Machakos yenye shughuli nyingi.

Waliongeza kwamba barabara hiyo ina manufaa kwa wananchi wa vijiji hivyo kwani ni njia fupi ya kuunganisha makwao ikilinganishwa na kutumia njia ndefu wanapotumia barabara ya Kivutini-Kyamwilu-Ngelani.