Mwanakandarasi asema ujenzi wa Kipchoge Stadium umekwama kwa kukosa pesa
MWANAKANDARASI mmoja sasa anasema kuwa uwanja wa michezo wa Kipchoge 64, Eldoret umekwama kutokana na hatua ya serikali ya kaunti ya Uasin Gishu ya kuchelewa kutoa pesa.
Haya yanajiri huku kamati ya bunge ikitaka uchunguzi ufanywe kuhusu mradi huo.
Kulingana na mwanakandarasi, hatua hiyo imesababisha mradi huo kukwama tangu 2023.
“Utekelezaji wa mradi huo umeathiriwa na kucheleweshwa kwa kutolewa kwa pesa na serikali ya kaunti. Haijategemewa katika malipo ya Sh120 milioni na kusababisha kukwama kwa mradi huo tangu Desemba 2023,’ alisema Mhandisi Denis Ongata, Msimamizi wa mradi huo.
Mradi huo ni miongoni mwa zile ambazo Kamati ya Seneti ya Uhasibu wa Umma (PAC) inataka kuchunguzwa na Tume ya Maadili na Kupambana na Ufisadi (EACC) kwa madai ya ubadhirifu wa rasilimali za umma.
Hospitali ya Ziwa Level Four yenye uwezo wa Sh600 milioni yenye vitanda 400 na kituo cha kutathmini mahitaji maalum ambacho kinatarajiwa kugharimu zaidi ya Sh2.4 bilioni pia ni mradi mwingine ambao umekwama.
Mwenyekiti wa kamati hiyo na seneta wa Homa Bay Moses Kajwang anataka EACC kuharakisha uchunguzi wa miradi hiyo ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi ya waliohusika na ubadhirifu wa fedha za umma.
Kamati iliitaka serikali ya kaunti kuwashirikisha wanakandarasi na kuharakisha kukamilisha miradi iliyotelekezwa.
“Pesa za walipa ushuru ziko hatarini na kaunti inafaa kumshirikisha mwanakandarasi kupitia fomula ya kurejea kazini na kuharakisha kukamilisha mradi huo,” akasema Johannes Mwaruma, seneta wa Taita Taveta na mwanachama wa kamati hiyo.
Alifichua kuwa mradi huo ulifadhiliwa awali chini ya Mpango wa Kenya Urban Support Program lakini baadaye ukachukuliwa na serikali ya kaunti baada ya kukamilika kwa kandarasi chini ya mpango huo.
“Utekelezaji wa mradi huo umekumbwa na changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na masuala ya kiufundi na matatizo ya kifedha,’ alisema Bw Koiyet huku akithibitisha kuwa kazi za ujenzi zimesitishwa kwa mwaka jana.