Binti Mfalme Zahra Aga Khan apokea tuzo ya juu kitaifa
RAIS Rais William Ruto amemtunuku Binti Mfalme Zahra Aga Khan tuzo ya Elder of the Order of the Golden Heart (EGH) kwa kutambua uongozi wake katika kuinua jamii nchini Kenya na kwingineko duniani.
Binti Mfalme Zara, alipokea tuzo hiyo katika hafla ya kupendeza iliyofanyika Ijumaa katika Ikulu ya Nairobi.
“Heshima hii inatambua uongozi wako wa kipekee na dhamira yako ya muda mrefu katika kuendeleza afya, elimu na maendeleo ya kijamii — nguzo kuu za utu na maendeleo ya pamoja,” alisema Rais Ruto alipokuwa akimpongeza.
Binti Mfalme Zahra ni mzaliwa wa kwanza wa marehemu Aga Khan IV na dada yake Aga Khan V. Alitunukiwa rasmi tuzo hiyo kupitia notisi ya Gazeti la Serikali iliyochapishwa Machi 2025.
Katika toleo hilo maalum, Rais Ruto pia alimtunuku Aga Khan V tuzo ya Chief of the Order of the Golden Heart (CGH), heshima ya juu zaidi ya kiraia nchini Kenya. Sherehe ya kumvisha nishani ilifanyika Agosti 2025.
“Ni kwa heshima kubwa na shukrani tele ninapokea tuzo hii adhimu leo,” alisema Binti Mfalme Zahra. “Ninaipokea kwa niaba ya wafanyakazi zaidi ya 15,000 wa AKDN na wengine wengi wa kujitolea wanaoishi hapa.”
Aliongeza kuwa familia yake ina historia ndefu nchini Kenya, akibainisha kuwa babake marehemu alijenga taasisi nyingi nchini katika sekta mbalimbali. Aga Khan IV alifariki Februari 2025.
Rais Ruto alikumbuka kwa shukrani urithi wa Aga Khan IV, akisema kujitolea kwake kuboresha maisha na ushirikiano wake wa karibu na Kenya tangu uhuru umeacha alama isiyofutika. Alieleza imani kuwa chini ya uongozi wa Aga Khan V, dhamira hiyo itaendelea kust