Habari

Godhana achukua uongozi wa Jumuiya ya Pwani

Na MWANDISHI WETU February 14th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

GAVANA wa Tana River, Dhadho Godhana, amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Jumuiya Ya Kaunti Za Pwani (JKP), kumrithi Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro.
Gavana Godhana anakuwa mwenyekiti wa nne wa jumuiya hiyo ya kiuchumi iliyoanzishwa rasmi mwaka 2014 ambayo afisi yake iko mjini Mombasa.
Pia Godhana ni mwenyekiti wa Kamati ya Usalama na Masuala ya Kigeni katika Baraza la Magavana (CoG).
Wanachama wa JKP ni kaunti za Mombasa, Kwale, Kilifi, Lamu, Taita Taveta na Tana River na lengo la muungano ni kukuza maendeleo kupitia rasilmali za pamoja na mipango ya kiuchumi.