Habari za Kaunti                                                
                                            
                                        Mbunge alalamikia ongezeko la shule za kibinafsi
 
                                                    
                                                        Picha yaonyesha madawati katika darasa moja.  Picha|Maktaba                                                    
                                                MBUNGE wa Mvita, Mohamed Soud amelalamikia ongezeko la shule za kibinafsi, katika eneobunge lake akionya kuwa hali hiyo inatishia shule za umma.
Mbunge huyo alisema ana wasiwasi kuwa kuongezeka kwa ghafla kwa shule za kibinafsi katika eneobunge lake kumefanya shule za umma kusalia bila wanafunzi licha ya serikali kuwekeza kwa manufaa ya wakazi.
Alitaja shule ya msingi ya Serani ambayo serikali iliwekeza ili kuongeza idadi ya wanafunzi kama mfano wa inayoathiriwa.