• Nairobi
  • Last Updated May 10th, 2024 10:55 PM
Nyeri: Wafanyakazi wa kaunti waagizwa kufunga baa zao

Nyeri: Wafanyakazi wa kaunti waagizwa kufunga baa zao

WAFANYAKAZI wa kaunti ya Nyeri wanaomiliki baa wamepewa notisi ya wiki moja kufunga biashara zao.

Akizungumza Ijumaa wakati wa kuidhinisha Mswada wa Kaunti wa Kudhibiti Vileo uliopitishwa na Bunge la Kaunti mwezi Februari na kuwa sheria, Gavana Mutahi Kahiga alisimamisha utoaji wa leseni mpya kwa wanaomiliki baa hadi mchakato wa uhakiki utakapokamilika.

“Hii ina maana kwamba katika kipindi cha wiki mbili zijazo, viongozi wote waweke ramani ya kila baa, namba za usajili, wamiliki na bidhaa zinazouzwa,” gavana Kahiga alisema.

  • Tags

You can share this post!

Mfanyabiashara akiri kumlawiti mwanamume mwenzake

Steve Mbogo: Serikali inamcheza Raila kuhusu uenyekiti AUC

T L