• Nairobi
  • Last Updated May 21st, 2024 9:55 AM
Wezi sugu watumia watoto kutekeleza uhalifu Riruta

Wezi sugu watumia watoto kutekeleza uhalifu Riruta

NA FRIDAH OKACHI

WEZI sugu katika mitaa mbalimbali jijini Nairobi sasa wanatumia mbinu mpya ya kuwatumia watoto na vijana wa umri chini ya miaka 18 kutekeleza uhalifu huo.

Katika wadi ya Riruta, msimamizi wa kituo cha polisi cha Riruta Sarah Kimsar amewataka wazazi kuwalinda na kuwapa ushauri watoto wao ili wasiingie katika mtego huo.

Hii ni baada ya visa kadhaa kuripotiwa kwamba watoto wamekuwa wakitumiwa na wezi sugu kutekeleza uhalifu.

“Tumepokea ripoti tatu kuhusu baadhi ya watoto waliotajwa kutumiwa na wezi kutekeleza wizi katika ploti za watu. Watoto hawa wanatumika kuingia katika ploti kisha kwa nyumba za wakazi ambapo wao huiba vitu vya thamani na kuwapelekea waliowatuma,” akasema Bi Kimsar.

Afisa huyo alisema baadhi ya watoto wanaofikishwa kituoni humo hudai kuwa hawaishi na wazazi wao.

“Wengi wa watoto wakiletwa husema kuwa ni mayatima na kwamba wanaishi na walezi, wajomba au shangazi,” aliongeza Bi Kimsar.

Bi Carolyne Miburo, ambaye huishi eneo la Kabiria lililoko Riruta, aliambia Taifa Jumapili kwamba alipoteza vifaa vya kielektroniki ikiwemo simu yake.

“Mwizi alikuwa ni mtoto aliyeingia katika ploti na wakazi wenzangu walimuona. Kusema ukweli baadhi ya wakazi walichukua hatua mikononi mwao wakamchapa na kumshurutisha atoe nambari ya simu ya babake. Unajua alitoa namba ya babake licha ya kwamba awali kwenye kituo cha polisi alikosa kutoa akidai yeye ni yatima,” akaeleza Bi Miburo.

Mkazi huyo alisema kuwa licha wa watoto hao kutumiwa, wengi hukwepa kwa kutaja wasiohusika.

“Wakati huyo mtoto alifikishwa katika kituo cha polisi, alianza kutoa taarifa za uongo,” akaongeza.

Mzazi wa mtoto huyo mmojawapo wa wanaotumika alisikitishwa na vitendo vya mwanawe ambaye aliiba Sh20,000 na simu ya jirani.

  • Tags

You can share this post!

Gachagua atambua ‘Uhuru ni mtoto wetu’

Uhuru, Gachagua wacheza ‘paka na panya’

T L