Habari za Kitaifa

Kenha yatoa muundo mpya wa Nithi Bridge, yasema itahitaji Sh7bn

Na GITONGA MARETE March 12th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

MAMLAKA inayosimamia Barabara Kuu nchini (KeNHA) imetoa miundo ya daraja jipya la Nithi, inayopigiwa debe kuwa moja kati ya vivuko maridadi na ghali zaidi kuwepo nchini itakapokamilika.

Likiwa na bajeti inayokadiriwa kufikia Sh7 bilioni, daraja hilo litameza nusu ya kilomita 84 za barabara kuu yenye mikondo miwili ya Kenol-Marua, ambayo gharama yake ya awali ilikadiriwa kuwa Sh14.6 bilioni.

Hata hivyo, kutokana na changamoto za ucheleweshaji na ununuzi, gharama ya mradi huo ilikadiriwa upya na kufikia Sh17 billion.

Barabara kubwa zaidi ya daraja nchini ni daraja la Mteza Creek, yenye kilomita 1.44, iliyojengwa kama sehemu ya mradi wenye thamani ya Sh27 bilioni wa Awamu ya Pili ya Barabara ya Dongo Kundu inayounganisha Mombasa na pwani kusini.

Muundo mpya wa daraja jipya la Nithi uliotolewa la Mamlaka ya Barabara Kuu (KeNHA). Picha|Pool

Kwa gharama ya Sh2.66 bilioni kwa kila kilomita, inakadiriwa kugharimu takriban Sh4 bilioni.

Hata hivyo, kwa Nithi, kutokana na gharama ya daraja inayotumika kwa sasa ikizingatiwa maisha yaliyokatizwa na uchungu ambao imewasababishia Wakenya hasa eneo la Mlima Kenya Mashariki, asasi za serikali zinaamini Sh7 bilioni si ghali.

Akihutubia wakazi wa Meru majuzi, Naibu Rais Kithure Kindiki alisema serikali imejitolea kukamilisha mradi huo kwa wakati uliopangiwa.

“Sasa tuna pesa na umma tayari umeshirikishwa kutoa maoni yake. Hivi karibuni, nitamleta mwanakandarasi kuanza ujenzi,” alisema Naibu Rais mjini Tigania Mashariki, mnamo Februari 25, 2026.