• Nairobi
  • Last Updated May 21st, 2024 7:05 PM
Mamia hatarini serikali ikipanga kutwaa ardhi zote za umma zilizonyakuliwa

Mamia hatarini serikali ikipanga kutwaa ardhi zote za umma zilizonyakuliwa

NA BARNABAS BII

HUENDA mamia ya watu wakafurushwa makwao huku serikali ikilenga kutwaa ardhi za umma zilizonyakuliwa kote nchini.

Hii inalenga kuwezesha utekelezaji wa miradi muhimu ya maendeleo, ikiwa ni pamoja na ujenzi wa nyumba za bei nafuu.

Rais William Ruto ametoa notisi kwa wawekezaji wa kibinafsi ambao wamenyakua ardhi ya umma kinyume cha sheria kuzisalimisha au wafurushwe kwa nguvu ili kuwezesha utekelezaji wa ajenda yake ya maendeleo katika ujenzi wa makazi, kuendeleza kilimo, ujenzi wa viwanda miongoni mwa mipango mingine.

Amewaagiza maafisa wa Wizara ya Ardhi na wasimamizi wa kitaifa na kaunti kuratibu urejeshaji wa mashamba ya umma yaliyonyakuliwa akibainisha kuwa kunapunguza kasi ya kuanzishwa kwa miradi muhimu ya maendeleo nchini kote.

“Wanyakuzi hao wa ardhi wana chaguo moja pekee, kusalimisha ardhi ya umma na kuhama kabla hatujachukua hatua,” alisema Dkt Ruto alipozuru Bonde la Ufa kuzindua miradi ya nyumba za bei nafuu.

 

 

 

  • Tags

You can share this post!

Gideon Moi alaani vikali mauaji dhidi ya wanawake

Mkenya azuiliwa Marekani kwa kudaiwa kumuua muuzaji kuni

T L