Habari za Kitaifa

Mashujaa Dei 2024: Kwa njia ya picha

Na SAMMY WAWERU October 20th, 2024 Kusoma ni dakika: 1

RAIS William Ruto, Jumapili, Oktoba 20, 2024 ameliongoza taifa kuadhimisha Mashujaa Dei mwaka huu.

Mashujaa Dei, ni siku ya kitaifa nchini Kenya, ambayo huadhimishwa kila mwezi Oktoba tarehe 20.

Aidha, ni Sikukuu ya umma kuwaheshimu na kuwatambua kwa pamoja wananchi waliochangia katika mapambano kupata uhuru wa Kenya au waliochangia kwa njia chanya kuboresha taifa baada ya uhuru.

Sherehe za Mashujaa mwaka huu, 2024 zinafanyika katika Gatuzi la Kwale, Uga wa Kwale.

Rais Ruto ameandamana na Naibu Rais mteule, Prof Kithure Kindiki aliyemlaki rasmi.

Kauli mbiu ya Mashujaa Dei 2024 ni ‘Boma yangu’, kwa Kiingereza ‘Affordable Housing’.

Ujenzi wa nyumba za bei nafuu, ni mojawapo ya sera za Dkt Ruto kupitia ajenda kuu ya BETA – Mabadiliko ya Kiuchumi ya Chini Juu.

Picha zifuatazo zinatoa taswira kamili ya jinsi hafla hiyo inayoendelea ilivyo:

Wananchi wakiingia alfajiri na mapema Kwale Stadium. PICHA|KEVIN ODIT
Gavana wa Mombasa, Bw Abdulswamad Nassir pamoja na baadhi ya viongozi kutoka Pwani wakiingia Kwale Stadium. PICHA|KEVI ODIT
Maafisa wa KDF wakipiga doria na mbwa kuimarisha ulinzi Kwale Stadium. PICHA|KEVIN ODIT
Wananchi waliofika Kwale Stadium wakikaguliwa na maafisa wa polisi. PICHA|KEVIN ODIT
Maafisa wa Kanjo Kwale kwenye gwaride. PICHA|KEVIN ODIT
Maafisa wa NYS kwenye gwaride. PICHA|KEVIN ODIT
Maafisa wa Magereza kwenye gwaride. PICHA|KEVIN ODIT
Timu ya watumbuiza kwa nyimbo za kiasili Pwani. PICHA|KEVIN ODIT
Baadhi ya mashujaa wanaotarajiwa kutambuliwa na kutuzwa na Rais Ruto. PICHA|KEVIN ODIT
Luteni Kanali Faith Mwagandi, aliyeongoza maafisa wa KDF kuadhimisha Mashujaa Dei 2024. PICHA|KEVIN ODIT