• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 11:13 AM
Mshukiwa mkuu wa ulanguzi wa mihadarati anaswa

Mshukiwa mkuu wa ulanguzi wa mihadarati anaswa

Na WINNIE ATIENO

MAAFISA wa upelelezi (DCIO) wamemkamata mwanamume anayeshukiwa kuwa mhusika mkuu wa ulanguzi wa dawa za kulevya.

Maafisa hao wanaoshika doria katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Moi, Mombasa, walimkamata Bw Salim Kalinga Mwinyi kuhusiana na madai hayo.

Maafisa hao pia walivamia nyumba ya mshukiwa huyo mtaa wa Magogoni, eneo la Kisauni, na kupatakilo moja ya heroini, bangi, mizani na Sh1.7 milioni pesa taslimu.

Maafisa wa polisi walisema fedha hizo ambazo inashukiwa kuwa zilitokana na biashara hiyo haramu, zilipatikana kwenye nyumba ya mshukiwa ambapo alikuwa akiendeleza shughuli hiyo ya ulanguzi pamoja na mkewe.

“Mnamo saa tisa usiku, maafisa wa DCIO kutoka kitengo cha doria katika uwanja wa kimataifa wa ndege ya moi walipata habari kuhusu mshukiwa Salim kalinga Mwinyi na kuvamia nyumba yake na kupata vitu hivyo,” taarifa kutoka idara ya polisi ilisema.

Makachero hao, walisema mshukiwa huyo amekuwa akishukiwa kwa ulanguzi wa dawa za kulevya anayehudumu eneo la Pwani.

Kulingana na maafisa hao, mshukiwa huyo alikuwa mpinzani wa kibiashara wa marehemu Swaleh Yusuf Ahmed, maarufu Kendereni.

Bw Ahmed alipatikana ameuawa wiki mbili zilizopita kwenye kisa ambacho maafisa wa polisi walikitaja kuwa uhasimu wa kibiashara.

Idara hiyo ya usalama ikiongozwa na Waziri Kithure Kindiki, ilipinga madai ya kuhusika na mauaji hayo wakiitaka familia yake kuwasilisha ripoti hiyo kwa uchunguzi.

“Kwenye biashara hiyo ya ulanguzi wa dawa za kulevya na usambazaji wa bidhaa hiyo, wawili hao walikuwa mahasimu wakubwa hasa katika eneo la Magodoroni na Arusini eneo la Kisauni,” ripoti ya usalama ilisema.

Maafisa wa polisi walidai kuwa Bw Mwinyi alikuwa akitumia wanafunzi wa shule wa kike hasawa familia yake, kusambaza mihadarati.

Polisi pia walisema kuwa wake wawili wa mshukiwa, wamewahi kukamarwa na kesi dhidi yao bado zinaendelea mahakakamani.

Mshukiwa huyo anatarajiwa kufikishwa mahakamani Jumatatu.

  • Tags

You can share this post!

Mwanablogu aliyeshtakiwa kuandika taarifa za kupotosha...

SOKOMOKO: Kujitetea kwa Murkomen kuhusu ajali barabarani...

T L