Pigo jingine kwa familia ya Raila dada yake akifariki akitibiwa hospitalini
FAMILIA pana ya aliyekuwa Waziri Mkuu Hayati Raila Odinga, imepata pigo jingine kufuatia kifo cha dadake mkubwa Berryl Achieng Odinga.
Kifo cha Achieng kilitangazwa na na dada yao mdogo, Ruth Odinga, ambaye alisema kuwa Berryl alifariki Jumanne, Novemba 25. Hata hivyo, hakufichua chanzo cha kifo hicho.
“Ni kwa moyo mzito lakini tukikubali mapenzi ya Mungu, tunatangaza kifo cha ghafla cha Beryl Achieng Odinga. Binti wa marehemu Jaramogi Oginga Odinga na Mama Mary Ajuma Oginga. Mama yake Ami Auma, Chizi na Taurus,” Ruth alitangaza.
“Ingawa tumehuzunishwa sana na kifo chake na pengo kubwa aliloliacha maishani mwetu, tunapata faraja tukiamini yuko salama mikononi mwa Bwana, na tunashukuru kwa zawadi ya muda tuliojaaliwa kushiriki naye,” aliongeza.
“Dada yake Seneta Oburu Oginga,Raila Odinga, Akinyi Wenwa, na Ruth Odinga, miongoni mwa wengine. Shemeji wa Dkt Anne Oburu, Dkt Canon Ida Odinga, Tabu Osewe na Judy Oburu.
“Ingawa tumegubikwa na huzuni kuu kutokana na kifo chake na pengo kubwa aliloacha maishani mwetu, tunapata faraja kwa kuamini kuwa sasa yuko salama mikononi mwa Bwana. Tunashukuru kwa zawadi ya muda tuliobarikiwa kuwa naye na kwa athari kubwa na ya kipekee aliyokuwa nayo kwa wote waliomfahamu,” alisema Ruth.