• Nairobi
  • Last Updated May 5th, 2024 6:07 PM
Supkem: Waislamu eneo la Pwani wamuunga Ole Naado

Supkem: Waislamu eneo la Pwani wamuunga Ole Naado

NA KNA

VIONGOZI wa baraza Kuu la Waislamu nchini (Supkem) eneo la Pwani wameapa kusimama na mwenyekiti wa baraza hilo Hassan ole Naado.

Wanasema kiongozi huyo alichaguliwa na wajumbe kutoka kaunti zote 47 miaka mitatu iliyopita.

Wakiongozwa na mwenyekiti wa baraza hilo tawi la Mombasa, Athman Akbar, waliapa kusimama na Sheikh ole Naado, walipomkataa Bw Yusuf Nzibo.

“Mwaka wa 2020, wajumbe wote walikataa uongozi wa Bw Nzibo. Alienda mahakamani kupinga uamuzi huo na kupoteza kesi. Kwa nini msajili wa vyama atulazimishe?” akauliza Bw Akbar.

  • Tags

You can share this post!

Savula abaki motoni washtakiwa 13 wakiachiliwa

Mtakuja kuelewa umuhimu wa kubariki mashoga – Papa

T L