Watu sita wafariki katika ajali ya helikopta Nandi
Watu sita wamefariki dunia kufuatia ajali ya helikopta iliyotokea jana jioni katika kijiji cha Chepkiep, wilaya ya Mosop, kaunti ya Nandi. Helikopta hiyo ililipuka na kuteketea baada ya kuanguka.
Kamanda wa Polisi wa Kaunti ya Nandi, alithibitisha tukio hilo na kusema kwamba hakuna aliyenusurika. Helikopta iliyohusika ni ya kampuni inayomilikiwa na shirika lililo na ofisi katika uwanja wa ndege wa Wilson, Nairobi.
Habari zaidi kufuatia