Habari za Kitaifa

Watu sita wafariki katika ajali ya helikopta Nandi

February 28th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

Watu sita wamefariki dunia kufuatia ajali ya helikopta iliyotokea jana jioni katika kijiji cha Chepkiep, wilaya ya Mosop, kaunti ya Nandi. Helikopta hiyo ililipuka na kuteketea baada ya kuanguka.

Kamanda wa Polisi wa Kaunti ya Nandi, alithibitisha tukio hilo na kusema kwamba hakuna aliyenusurika. Helikopta iliyohusika ni ya kampuni inayomilikiwa na shirika lililo na ofisi katika uwanja wa ndege wa Wilson, Nairobi.

Habari zaidi kufuatia