Habari

Kalonzo aapa kuwasilisha kesi ya kusimamisha ubomoaji wa nyumba Mavoko

Na STANLEY NGOTHO February 1st, 2026 Kusoma ni dakika: 2

KIONGOZI wa Chama cha Wiper, Kalonzo Musyoka, amejiunga na mzozo wa ardhi unaohusisha Benki ya Kenya Commercial Bank (KCB) na mamia ya wamiliki wa nyumba wanaokabiliwa na tishio la kufurushwa katika eneo la Mavoko, Kaunti ya Machakos.
AkizungumzaJanuari 31, 2025 akiandamana na viongozi wa muungano wa upinzani, Bw Musyoka alisema upinzani utatumia njia za kisiasa na kisheria kuzuia kile alichokitaja kuwa mpango wa haraka na haramu wa kuwafurusha wakazi hao.
Alidai kuwa mawakala wa KCB wamekuwa wakiwatoza wakazi bei ya juu mno ili kununua ploti wanazoishi, huku nyumba kadhaa tayari zikiwekewa alama kubomolewa.
 “Tumeelekeza mawakili wetu kwenda mahakamani kusimamisha kufurushwa kwa nguvu kwa watu wetu kunakoendeshwa na utawala wa William Ruto,” alisema Bw Musyoka, akidai kuwa kuna mpango wa kutumia polisi kusimamia ubomoaji na kufurusha wakazi.
 Kiongozi huyo wa Wiper alimwagiza Naibu Kiongozi wa Wachache katika Bunge la Kitaifa na Mbunge wa Kathiani, Robert Mbui, kuwasilisha hoja bungeni kuhusu kile alichokiita mchakato wa uuzaji ardhi usio wazi.
“Hapo awali wakazi waliambiwa walipe Sh200,000 kama amana ili kuhifadhi ardhi wanakoishi. Tunataka KCB itoe maelezo ni wangapi wamelipa, na  Mkutano wa awali wa usalama ulioitishwa na Naibu Kamishna wa Kaunti Ndogo ya Mavoko, Otieno Odidi, ulifutiliwa mbali baada ya kubainika kuwa ungejumuisha wanasiasa.
Bw Musyoka pia alishutumu serikali kwa kulenga maeneo yanayounga mkono upinzani, akihusisha mvutano wa ardhi Mavoko na ubomoaji wa hivi karibuni katika ardhi ya Kampuni ya Simiti ya East African Portland Cement (EAPC).
“Baada ya kuharibu nyumba za thamani ya mamilioni katika ardhi ya EAPC, sasa wanahamia ardhi ya KCB ili kumuadhibu Gavana wa Machakos, Wavinya Ndeti, kwa msimamo wake wa kisiasa,” alidai
 Aliyekuwa Waziri wa Utumishi wa Umma, Justin Muturi, aliwahimiza wakazi kupinga kile alichokitaja kama hila za serikali.
 “Serikali inatumia KCB kuwanyang’anya wananchi mali zao. Hili lazima likome, la sivyo tutaitisha maandamano ya kitaifa,” alisema Bw Muturi.
 Kiongozi wa Chama cha DAP-K, Eugene Wamalwa, aliunga mkono kauli hizo.
Mbunge wa Mavoko, Patrick Makau, ambaye amekuwa mkosoaji mkubwa wa mpango wa kuwafurusha wakazi, hakuhudhuria mkutano huo.
 Hata hivyo, meneja wa mradi wa KCB, Njoroge Njuguna, alisema wiki mbili zilizopita kuwa benki ilipatia kipaumbele wakazi walio katika ardhi lakini baadhi yao walishindwa kutimiza masharti.
“Tuko tayari kuzungumza na watu binafsi kuhusu mipango nafuu ya malipo. Wchache hawataki kufuata masharti,” alisema, akiongeza kuwa ardhi hiyo sasa iko wazi kuuzwa kwa umma kwa misingi ya mnunuzi na muuzaji aliye tayari.