Habari

Kanja aagiza konstebo Mukhwana ashtakiwe kwa mauaji ya Ojwang

Na FATUMA BARIKI June 12th, 2025 Kusoma ni dakika: 1

INSPEKTA Jenerali wa Polisi Douglas Kanja ameagiza afisa wa polisi katika kituo cha Central, Konstebo James Mukhwana ashtakiwe kwa mauaji ya mwalimu na bloga Albert Ojwang.

Kwenye hati ambayo Taifa Leo imeona, IG Kanja anasema Bw Mukhwana alikamatwa Alhamisi, Juni 12, 2025 na kuzuiliwa katika kituo cha polisi cha Capitol Hill akisubiri kufunguliwa mashtaka.

Kumekuwa na shinikizo, ikiwemo maandamano ya kutaka afisa wa ngazi za juu kwenye kikosi cha polisi awajibike kwa kifo cha Ojwang mikononi mwa polisi.