Maandamano yashika kasi jijini Nairobi kumtaka Lagat ajiuzulu
MAMIA ya vijana wanaandamana katika barabara za jiji kuu la Nairobiwakimtaka Naibu Inspekta Jenerali wa Polisi Eliud Lagat ajiuzulu.
Maandamano hayo yanatishia kuathiri shughuli nyingi muhimu ndani ya jiji, huku Wakenya wakisubiri hotuba ya bajeti ya mwaka wa kifedha 2025/2026 kutoka kwa Waziri wa Fedha, John Mbadi.
Waandamanaji wanazunguka katika barabara muhimu huku polisi wakiwarushia vitoa machozi kuwazuia wasifike makao ya bunge.
Baadhi walisikika wakiimba wantam.
Pia walifunga barabara kuu kama Harambee Avenue, jambo lililotafsiriwa kama jaribio la kupenya ulinzi mkali uliowekwa kuzunguka Bunge.
Polisi walitumia vitoa machozi na mbinu nyingine za kudhibiti umati kuwatawanya waandamanaji.
Baadhi ya waandamanaji walionekana wamevalia mavazi ya rangi za bendera ya Kenya, huku wakiimba kwa sauti ya pamoja wakishinikiza kujiuzulu kwa Naibu Inspekta Jenerali kufuatia kifo cha mwanablogu, Albert Ojwang, aliyefariki akiwa
Watumiaji wa barabara ya Thika waliripoti ukaguzi mkali ambapo maafisa walikuwa wakikagua magari kwa makini ili kupunguza idadi ya magari yanayoingia CBD.
Baadhi ya biashara zimefungwa kwa hofu ya uporaji.
Licha ya ulinzi mkali, waandamanaji walionekana kuwa thabiti wakiendelea kuandamana kupitia barabara mbalimbali katikati kwa jiji..
Haya yalijiri wakati viongozi wakuu wa Huduma ya Kitaifa ya Polisi (NPS), wakiongozwa na Inspekta Jenerali Douglas Kanja na Mkuu wa DCI Mohamed Amin, wakiwa mbele ya Kamati ya Bunge ya Usimamizi na Usalama wa Ndani kujibu maswali kuhusu kifo cha Ojwang.