Habari

Matangazo ya BBC: polisi wawili waagizwa kufika kortini

Na RICHARD MUNGUTI May 30th, 2025 Kusoma ni dakika: 1

MAAFISA wawili wa polisi wameagizwa wafike kortini kueleza sababu hawajakamilisha uchunguzi katika kesi ambapo washukiwa wanne wanachunguzwa kwa utayarishaji wa filamu kuhusu shambulizi la Gen-Z mwaka uliopita ambapo zaidi ya waandamanaji 30 waliuawa na polisi.

Hakimu mwandamizi Eric Otieno Wambo aliwaamuru Inspekta Nickson Kinywa na Mogah Wekesa Wechuli kufika kortini Juni 16,2025 kueleza ikiwa wamekamilisha uchunguzi au la dhidi ya washukiwa hao wanne.

Bw Wambo alitoa agizo hilo wakati wa kutajwa kwa kesi dhidi ya 25,2025 are Nicholas Wambugu, Brian Adagala, Mark Denver Karubiu na Christopher Wamae wanaodaiwa walitayarisha filamu iliyopeperushwa na shirika la utangazaji la kimataifa la Uingereza –BBC- Aprili 2025.

Katika taarifa hiyo ya BBC video jinzi wanaharakati walivyouawa na polisi katika majengo ya bunge mnamo Juni 25,2024.

Wakili Ian Mutiso anayewakilisha washukiwa alisema miezi zaidi ya miwili imepita na polisi hawajakamilisha.

Mbali na kuomba polisi waeleze siku ya kukamilisha uchunguzi mshtakiwa pia Bw Mutiso aliomba dhamana ya Sh10,000 pesa tasilimu waliyoachiliwa washukiwa hao wasalie nje kwa masharti hay ohayo.

“Kufuatia ombi la washtakiwa naamuru kesi hii itajwe Juni 16,2025 na kuwaamuru maafisa wanaochunguza kesi hii wafike kortini kueleza tamati ya zoezi lao,”Bw Wambo aliagiza.

Washukiwa hao wanne (4) wameagizwa warudi kortini Juni 16,2025 kwa maagizo zaidi.