Habari
Mbunge wa Juja George Koimburi atekwa nyara na kutupwa Kibichoi

Picha aina ya 'screengrab' inayoaminika kuwa ya Mbunge wa Juja George Koimburi baada ya kupigwa na kutupwa eneo la Kibichoi, Kiambu. Picha|Hisani
MBUNGE wa Juja George Koimburi, ambaye alitekwa nyara Jumapili jioni amepatikana ametupwa Kibichoi, Kiambu, familia yake imethibitisha.
Kulingana video moja inayosambazwa mitandaoni, mbunge huyo anaonekana mwenye mavune huku akigaragara chini msituni ambako pia nguo zake zinaonekana kuwa na matope na kwingine kuraruka.
Familia yake imesema wamemkimbiza hospitalini kwa matibabu huku habari za kutekwa kwake zikipokewa kwa mshtuko na wafuasi wake hasa wale wanaoegemea mrengo wa aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua.
Taarifa zaidi ni kama tunavyozipokea…