Habari

Mbunge wa Juja George Koimburi atekwa nyara na kutupwa Kibichoi

Na MWANDISHI WETU May 26th, 2025 Kusoma ni dakika: 1

MBUNGE wa Juja George Koimburi, ambaye alitekwa nyara Jumapili jioni amepatikana ametupwa Kibichoi, Kiambu, familia yake imethibitisha.

Kulingana video moja inayosambazwa mitandaoni, mbunge huyo anaonekana mwenye mavune huku akigaragara chini msituni ambako pia nguo zake zinaonekana kuwa na matope na kwingine kuraruka.

Familia yake imesema wamemkimbiza hospitalini kwa matibabu huku habari za kutekwa kwake zikipokewa kwa mshtuko na wafuasi wake hasa wale wanaoegemea mrengo wa aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua.

Taarifa zaidi ni kama tunavyozipokea…