Habari

Mwandishi, mwanamageuzi mtajika Ngugi wa Thiong’o aaga dunia

Na MWANDISHI WETU May 28th, 2025 Kusoma ni dakika: 1

MWANDISHI mtajika duniani na mwanamageuzi Ngugi wa Thiong’o ameaga dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu nchini Amerika, familia yake imethibitisha.

Bw Ngugi ambaye anachukuliwa kuwa mwandishi mahiri zaidi wa riwaya Afrika Mashariki amekuwa nchini Amerika kwa miaka mingi na katika miaka ya hivi punde amekuwa akilemewa na maradhi.

Ripoti zinasema alikufa kwa mshtuko wa moyo.

Mwanawe, Mukoma wa Ngugi, aliandika kwenye safu yake mtandaoni:

“Nimejawa na majonzi kusema kwamba babangu, Ngugi wa Thiong’o alikata roho mapema leo (Jumatano, Mei 28, 2025). Singekuwa mimi nilivyo kama mwanawe, msomi na mwandishi bila yeye. Nampenda. Sijui itakavyokuwa kesho. Hayo tu ndio naweza kusema kwa sasa,”

Habari zaidi ni kadiri tunavyozipokea…