Pigo kwa Ruto jopo la fidia likiharamishwa
JOPO lililoteuliwa na Rais William Ruto kuchunguza na kupendekeza kulipwa fidia kwa wahanga waliojeruhiwa wakati wa ghasia za maandamano na dhuluma za polisi limepata pigo kubwa baada ya Mahakama Kuu kusitisha utendakazi wake.
Jaji Dennis Kizito Ngw’ono Mongare alipiga breki jopo hilo linaloongozwa Mtaalamu wa masuala ya kisheria Profesa Makau Mutua hadi pale kesi iliyowasilishwa na wakili Levi Munyeri itakaposikizwa na kuamuliwa.
Jaji Mong’are alisitisha kazi ya jopo hilo lililoteuliwa wiki iliyopitaa hadi Oktoba 10,2025 kesi hiyo itakaposikizwa.
Jaji huyo aliratibisha kuwa ya dharura kesi hiyo iliyoshtakiwa na Bw Munyeri anayedai Rais Ruto aliukiuka sheria kuteua jopo hilo kabla ya wahasiriwa kujulikana na majeraha waliyopata kutathminiwa na watalaam wa afya.
Mnamo Agosti 25 2025 Rais Ruto aliteua jopo la wanachama 14 akiwamo Rais wa Chama cha Wanasheria Nchini (LSK) Faith Odhiambo kuchunguza na kubaini idadi ya watu waliopigwa risasi na polisi na kujeruhiwa.
Haya yalitokea wakati wa maandamano ya kupinga sheria ya Fedha 2024/2025 na wakati wa kumbukumbu ya wahasiriwa wa dhuluma za polisi wa Juni 18/20.2024.
Mbali na wahasiriwa hao wa hivi majuzi pia jopo hilo lilitwikwa jukumu la kuwatambua wahasiriwa wa waamandamano ya hapo awali kwa lengo la kuwalipa fidia.
RaiS aliitaka jopo hilo kwa kushirikiana na vyombo vingine vya kisheria, litoe mapendekezo ya kiwango cha pesa amabazo wahasiriwa watalipwa na wakati huo huo kutoa mapendekezo kwa Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP) kuhusu wale wanaopasa kufunguliwa mashtaka kortini.