Habari

Ruto: Siwezi kuachia mamlaka kiongozi yeyote aliye upinzani kwa sasa

Na SHABAN MAKOKHA June 15th, 2025 Kusoma ni dakika: 1

RAIS William Ruto ameapa kutopeana mamlaka kwa kiongozi yeyote aliye upinzani kwa sasa akisema wote wamechanganyikiwa na hawana ajenga kwa nchi.

Rais Ruto amesema Upinzani wanatafuta kitu kimoja tu, yaani kumwondoa mamlakani bila mipango yoyote mahsusi kwa manufaa ya Wakenya na maendeleo kwa nchi.

“Nimeona ajenda yao kuu ni ‘Ruto must go’. Hakuna kingine. Sasa, ‘Ruto must go’ itasaidiaje Wakenya wanaokumbwa na changamoto za matibabu, elimu na matatizo mengine?” akauliza alipohudhuria ibada ya kanisa katika Shule ya Kivaywa, Lugari, Kaunti ya Kakamega.