Habari

Ubongo wa Boniface Kariuki umefariki, familia yasema

Na MWANDISHI WETU June 29th, 2025 Kusoma ni dakika: 1

BONIFACE Kariuki, mchuuzi aliyepigwa risasi kichwani, ubongo wake umefariki, familia yake imesema.

Kulingana na msemaji wa familia Emily Wanjira, walipokea simu saa sita usiku wa kuamkia Jumapili na kupewa habari hizo.

“Shina la ubongo limekufa kabisa, wasiwasi tulio nao sasa ni kwamba labda moyo pia utaacha kupiga. Tunachotaka ni haki kwa mtoto wetu,” akasema.

“Tunaomba tusaidiwe na hiyo bill,” akasema babake Boniface, Jonah Kariuki akionekana kuwa na wasiwasi mwingi, punde baada ya msemaji kuzungumza na wanahabari.

Alhamisi, familia iliambiwa kwamba kulikuwa na mabaki ya risasi kwenye ubongo wa Boni.

“Waliita risasi maalum. Inamaanisha wakati inafyatuliwa, inatawanyika mara tatu. Tuliambiwa haya na madaktari Alhamisi,” akafafanua. Alisema madaktari wamekuwa wakifanya kila wawezalo kuokoa maisha ya kijana huyo.

Boniface alipigwa risasi kwa kutumia bunduki aina ya shortgun, alisema msemaji.

Kwa ufafanuzi, bunduki aina ya shortgun ni ile inayotumika kuua wanyamapori au makabiliano na wavunja sheria.