Ufafanuzi kuhusu marufuku ya kula kwa kijiko na uma Mombasa
TAARIFA kuhusu Bunge la Kaunti ya Mombasa kupiga marufuku matumizi ya vyombo vya kulia chakula kama vile vijiko, uma na visu katika migahawa yote ndani ya Kisiwa cha Mombasa ilikuwa ni kichekesho cha siku ya ‘April Fools’.
Hatua hiyo haikutekelezwa na Bunge la Kaunti wala hakuna sheria yoyote halali kama hiyo iliyopitishwa.
Taarifa hiyo kwenye gazeti la Aprili 1, ilikusudiwa kuwa ya kichekesho, na haimaanishi kwamba kuna mabadiliko yoyote katika sera za kaunti kuhusu mitindo ya kula chakula katika Kisiwa cha Mombasa.