• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 5:07 PM
AFYA: Faida za kiafya kuyala machungwa

AFYA: Faida za kiafya kuyala machungwa

Na MARGARET MAINA

[email protected]

Mmeng’enyo wa chakula

KUTOKANA na kuwa na kiwango kikubwa cha nyuzinyuzi ‘fibre’, chungwa husaidia usagaji wa chakula tumboni na humpa afueni mtu mwenye matatizo ya tumbo.

Shinikizo la damu

Virutubisho vya Magnesium vilivyomo kwenye chungwa husaidia kuondoa tatizo la shinikizo la damu la juu (high blood pressure), hivyo machungwa ni mazuri kwa wagonjwa wa presha.

Ugonjwa ya mapafu

Chungwa pia lina kiasi kikubwa cha Vitamini B6 na Madini ya Chuma, virubisho ambavyo ni muhimu kwa uzalishaji wa seli nyekundu za damu, ambazo hufanya kazi ya kusafirisha hewa ya oksjeni mwilini, hivyo kuwa muhimu kwa kujikinga na ugonjwa wa mapafu.

Mifupa na meno

Chungwa lina kiasi kingi cha madini ya Calcium ambayo ni muhimu kwa uimarishaji wa mifupa na meno.

Afya ya ngozi

‘Anti-oxidants’ iliyomo kwenye chungwa, hutoa kinga kwenye ngozi ili isiharibike au kushambuliwa na magonjwa ya ngozi yanayoweza kujitokeza kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa. Pia huifanya ngozi ‘isizeeke’.

Lehemu

Virutubisho vilivyomo kwenye chungwa, hasa kwenye ngozi yake, hupunguza kiwango cha mafuta mabaya mwilini (bad cholesterol).

Kinga ya mwili

Vitamini C iliyomo kwenye chungwa huimarisha uzalishaji wa seli nyeupe ambazo ni muhimu kwa uimarishaji wa kinga ya mwili. Unapokuwa na kinga imara, huwezi kusumbuliwa na magonjwa mara kwa mara.

Mafua

Kutokana na wingi wa virutubisho vya kinga vilivyomo kwenye chungwa, ulaji wake mara kwa mara utakuepusha na magonjwa yanayoambukizwa na virusi kama vile mafua.

  • Tags

You can share this post!

DOMO KAYA: Koffi ashaomba radhi jamani, tuache unafiki

KRU yasimamisha msimu 2019-2020 kwa sababu ya COVID-19

adminleo