Na MISHI GONGO
Idadi ya walaji: 4
Viungo
Jinsi ya kutayarisha
Chukua unga wa ngano, hamira, sukari, chumvi na mafuta ya uto kisha changanya.
Ongeza yai na maziwa katika mchanganyiko na ukande hadi unga ulainike.
Tengeneza donge kisha uache uumuke.
Ukishaumuka kata unga kidogo kisha tengeneza kama rolls au minyororo.
Lingalinga mnyororo kwa soseji kisha panga kwa treya ya kuoka.
Oka kwa muda wa dakika 10.
Unaweza ukapakua ukala chakula hiki huku ukinywa ama sharubati ya machungwa au chai.