Namna suala la ubabedume limeangaziwa katika riwaya ya ‘Nguu za Jadi’
JUMA hili tunaangazia taasubi za kiume kwa kurejelea dondoo lifuatalo:
“Nyinyi mna maswali mengi. Si mngoje kwanza nimalize kusimulia halafu mniulize maswali?”
(a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
Msemaji – Sauni
Wasemewa – Lonare na Sagura.
Mahali – Nyumbani kwa Lonare
Kiini – Sauni alikuwa akiwasimulia kisasili kuhusu mwanamke mmoja aliyekuwa na hulka ya Sihaba ila Sagura na Lonare walikuwa wakimkatiza kila alipojaribu kuwasimulia kuhusu namna Mungu alivyojaribu kumtafutia Adamu mke. (Uk.81).
(b) Taja mbinu anayotumia Sauni kuendeleza riwaya.
Mbinu rejeshi/kisengere nyuma.
Hadithi ndani ya hadithi.
(c) Kisa hiki kinadhihirisha suala la ubabedume/taasubi za kiume katika nchi ya Matuo. Thibitisha kwa kurejelea riwaya ya ‘Nguu za Jadi’.
Ubabedume ni hali ya kuichuku lia jinsia ya kiume kuwa bora kuliko ya kike. Hali hii hujidhihirisha kupitia kwa matatizo yanayowakumba wanawake.
Mangwasha alinuia kufisha uhasa ma wa kikabila uliokita mizizi kati ya Wakule na Waketwa lakini nafasi yake katika jamii haikumruhusu. (Uk.7-8).
Inasemekana kuwa jamii hii ilishiba ubabedume na mwanamke wa kawaida asiyekuwa na cheo wala fulusi hakuwa na uso wa kuongea na wakuu wenye mamlaka nchini (Uk7-8).
Mangwasha alikuwa na nia ya kuwajuza watu kuhusu majungu yaliyopikwa na Chifu Mshabaha lakini alichelea kutokana na minyororo ya utamaduni ambayo haikumruhusu kuwahutubia watu. (Uk.11).
Mangwasha alilalamika kuwa mafunzo ya makungwi yalinuia kuwafunza wanawake kuyakubali mambo bila kuyasaili na bila kero. (Uk.32).
Mrima alimdunisha mkewe kwa kusema kuwa wanawake wana maneno mengi kama chiriku.
Aliamini kuwa mwanamke hapaswi kumuuliza mume anakotoka. Pia alimwambia mkewe kuwa mke akishaolewa yake huwa yamekwisha (Uk 40).
Mrima alimwambia Mangwasha kuwa ngamia hamei pembe na shingo haipiti kichwa (Uk 40).
Mrima alimjulisha Mangwasha kuwa hawezi kumzuia kuoa mwanamke mwingine kwa kuwa yeye ni mwanamume anayeweza kuoa wakati wowote na idadi yoyote ya wanawake (Uk 41).
Mangwasha anapoitetea nafasi yake kama mwanamke, alimwambia Mrima kuwa yeye ni mwenzake na wala si mtumwa wake (Uk 42).
Mangwasha alikumbuka kuwa hafai kuwahutubia wanaume kulingana na utamaduni wao lakini alikaidi mila za kwao na kuwahutubia watu (Uk 74).
Mbungulu na Mangwasha walipo gundua kuwa Sagilu alihusika na usambazaji wa vijikaratasi vya ku wafurusha Waketwa, Mbungulu alimwambia Mangwasha akae mbali na Sagilu na kuwa aache wazee walishughulikie suala hilo. (Uk.79-80).
Sauni alisema kuwa aliwahi kusoma kisasili cha Waebrania kilichoudhi na kumfanya mtu kuwachukia wanawake. (Uk.74).
Ngoswe alimwambia Mashauri kuwa wanawake ni wengi duniani mradi awe na pesa (Uk.124).